Viwawa ni chama cha Vijana Wakatoliki Wafanyakazi Tanzania, kwa lugha ya Kiingereza (Tanzania Young Catholic Workers Movement – T.Y.C.W), ni Chama cha Kitume cha Vijana ambao wanatumwa na Kanisa ili kuendeleza kazi aliyoianza Kristu Yesu. VIWAWA ni Chama cha Vijana na kinaendeshwa na Vijana wenyewe